Swahili articles

WOSIA KWA WANANDOA by Ferdinand Majimbo

todayMay 30, 2023 258 1 5

Background
share close

NDOA ni kuvumiliana na bila uvumilivu ndoa haiwezi kufaulu. Kuvumilia

kunamaanisha kukubali hali mbaya na ngumu ambazo hazifurahishi mtu.

Hasa, hali hizi huwa ni ngumu na nzito sana zinazoumiza mtu. Ni hali

ambazo mtu huwa hakuwa amezoea kabla ya kuingia katika ndoa au

kutarajia kupata katika ndoa. Baadhi ya shida huwa zinasababishwa na

mchumba wake au kuzuka kutokana na hali ambazo haziepukikikamwe.

Mtu pia anaweza kusababisha hali ngumu katika ndoa yake.

Ingawa wanandoa wanafaa kuvumiliana, kiwango cha uvumilivu na

mipaka yake pia kinapaswa kuzingatiwa ipasavyo.

Kuna shida zinazoweza kuvumiliwa kwa muda mrefu hadi hali ibadilike

na kuwa bora na kuna zile ambazo hata zikivumiliwa mtu hawezi kupata

afueni. Wakati mwingine watu huwa wanavumilia hali ambazo

zinawaweka kwenye hatari na kwa kufanya hivyo uvumilivu wao huwa

wa upofu.

Kuvumilia mume au mkeo akiwa mgonjwa au akipoteza kazi ni jambo

nzuri na la kupongezwa. Hii ndiyo aina ya uvumilivu wa kiapo cha ndoa.

Huu ni uvumilivu unaotokana na mapenzi ya dhati, pale mume na mke

wanasaidiana huku wakipitia hali ngumu ya uchumi na maradhi. Itakuwa

kukiuka kiapo cha ndoa iwapo sio ukatili mtu kuacha mumewe au

mkewe akiwa mgonjwa akisema amekuwa mzigo kwake. Lakini hii ni

tofauti na mtu kuvumilia mtu anayemtesa kimakusudi hima kimwili au

kisaikolojia. Kuna watu wanaovumilia kushambuliwa kimwili na

kisaikolojia na wachumba wao hadi wanaathirika kiafya na hata

kulemazwa. Kuvumilia mateso ya aina hii ni kilele kikubwa cha

upumbavu.

Kuna wanaume na wanawake wanaovumilia mateso kutoka kwa

wachumba wao hadi kaburini na kuwaacha waliowatesa wakiendelea na

maisha.

Katika kisa kimoja, mwanamke alivumilia madharau ya mumewe

kuwaleta wanawake tofauti kulala nao katika kitanda cha ndoa huku

akiamrishwa kulala kwenye kochi. Hatimaye mwanamume huyo

aliambukizwa Ukimwi na kufariki akiwa amepitisha kwa mkewe. Kama

mwanamke huyo hangevumilia kijinga na kujiondoa katika ndoa,

pengine hangejipata katika hali ya kuhuzunisha ya kuachwa mjane

anayeishi na Ukimwi.

Hata kama uvumilivu ni muhimu katika ndoa, unafaa kukitwa kwa busara

na hekima, haufai kuwa wa kienyeji tu eti kwa kuheshimu kiapo cha

ndoa. Itakuwa ujinga kuheshimu kiapo cha ndoa yako na mtu ambaye

hakiheshimu na hakuheshimu.

Vumilia ndoa yako na mtu anayekuheshimu lakini usivumilie katili

anayeweza kukupeleka kaburini na kuachwa akiendelea kufurahia

maisha yake kana kwamba haukuwahi kuwa katika maisha yake au

katika dunia hii.

Maisha ni yako na yake ni yake, kinachowaunganisha ni upendo na

kukutumbukiza katika mateso kunaonyesha upendo wake kwako

umetoweka.

Mambo ni mawili; waume wapende wake zao, wawajibike na kuheshimu

ndoa iwapo wanataka wawavumilie hali ngumu zinapozuka. Wake nao

waheshimu waume zao hata wakiwa wadhaifu na katika mazingira haya

ndoa zidumu na kuwa na furaha kwao wote

NA IKUMBUKWE SIKU ZOTE KWAMBA HESHIMA SIYO UTUMWA.

Written by: 254 Radio

Rate it

Previous post

Uncategorized

Eric Omondi asks for Play 75% Kenyan music

The Kenyan music industry has for ages been exclusive, with less than 20% of original Kenyan music being played across the various media platforms, stiff competition from countries like South Africa, Tanzania and Nigeria whose music industries are thriving has made it that much more difficult to traverse the space. On top of that, the conditions afforded to players in the industry are laughable. For years artists have had to […]

todayNovember 18, 2022 280 3

0%